Posts

UREJESHAJI KATIKA LUGHA YA KISWAHILI

UREJESHAJI KATIKA TUNGO ZA KISWAHILI swali hili linatutaka kujadili ni kwa namna gani urejeshi unavyojitokeza katika tungo mbalimbali za lugha ya Kiswahili. Katika utangulizi tumeweza kutoa fasili mbalimbali kulingana na wataalamu tofautitofauti kisha kiini cha swali ambacho tumeonyesha ni kwa namna gani urejeshi unavyojitokeza katika baadhi ya tungo za lugha ya Kiswahili. katika hitimisho tukatoa majumuisho kuhusiana na mjadala wa swali. Tukianza na fasili za dhana mbalimbali katika swali kama ifuatavyo;- TUKI (1990) wanaeleza kuwa urejeshi ni kitendo cha kuweka kiwakilishi ambacho huweza kutumiwa kupatanisha kishazi, kinachorejelea na kuvumisha kikundi nomino. yaani kishazi rejeshi kinafanya kazi ya kuvumisha nomino katika kikundi nomino hicho. Massamba (2009) anaeleza kuwa kishazi rejeshi ni kishazi ambacho kina uamilifu wa kurejelea kwenye kirai nomino ambacho kinakibeba. Anafafanua kwamba kishazi bebwa ni kishazi ambacho hakiwezi kujitegemea chenyewe na ambacho kimechopekwa nda...

UKUMUSHI KATIKA VITENZI VYA KISWAHILI

Kiswahili ni lugha ukumushi wa baada ya kikumushwa. Hata hivyo, kuna nyakati ambapo utaratibu huu hukiukwa. Kwa kutumia sintaksia ya vitenzi vya Kiswahili, thibitisha au pinga dai hili. Swali hili imegawanyika  katika sehemu kuu nne, sehemu ya kwanza utangulizi ambayo imebeba dhana za msingi katika kazi kulingana na wataalamu mbalimbali, kiini amabapo sehemu hii tumejadili swali pia hitimisho na marejeleo tuliyoyatumia katika kazi hii. Kwa kuanza na utangulizi dhana ya ukumushi imeelezwa kulingana na wataalamu mbalimbali kama ifuatavyo; Khamisi na Kiango (2002:58) wanaeleza dhana ya ukumushi kuwa ni maneno ambayo siyo vivumishi kwa asili, lakini hufanya kazi kama vivumishi yaani kazi ya kukumusha (kuongeza sifa au taariafa muhimu. Wanaendelea kwa kusema kuwa vikumushi siyo vipashio vilivyo katika kiwango cha neon tu, bali ni pamoja na makundi ya maneno ambayo katika kiwango cha kirai au kishazi. Chuo Kikuu Cha Oxford (2005) hueleza kuwa kikumushi ni neno ambalo linaweza kuwa k...

Sifa za Sanaa za Maoneshoo

Ni zipi sifa za sanaa za maonesho ya kiafrika? Dhana inayotendeka Uwanja wa kutendea Watendaji Hadhira kusudio la kisanaa muktadha wa kisanaa ubunifu

SIFA ZA USHAIRI WA KIJADI

Ushairi ni nini? Ni sanaa ya lugha ya mkato yenye ubunaji inayosawiri au kueleza jambo kwa hisi, hali au maono kwa namna yenye kuvutia hisia  na katika mpangilio wa maneno yenye urari wa wizani. Ushairi wa kijadi unasifa zifuatazo;  Madondoo haya machache yanaonesha mtazamo wa washairi wa Kiswahili au wakijadi kuhusu maana ya ushairi Ushairi ni wimbo Wenye maneno ya hekima Wenye lugha ya mkato wenye lugha nzito wenye urari wa vina na mizani wenye hisia ( mguso wa moyo)

AINA KUU ZA FASIHI NA TOFAUTI ZAKE

 Fasihi simulizi ni istilahi inayotumiwa na kueleza dhana ya fasihi itolewayo kwa mdomo bila kuandikwa. Istilahi hii ilizuka miaka ya 1970. Fasihi simulizi ni sanaa inayotungwa au kubuniwa kwa kichwa na kuwasilishwa kwa mdomo bila kutumia maandishi. Hivyo fasihi simulizi simulizi ni tukio linalofungamana na muktadha fulani wa kijamii (Mulokozi 2017:37-38) Fasihi simulizi ni sanaa ya lugha inayotungwa na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia ya maandishi. Kuwapo kwa fasihi andishi hutegemea mambo matatu ambayo ni mtunzi (ambaye kwa kawaida ndiye mwandishi), hadhira (wasomaji) na mdhamini ambaye ni mchapishaji atakayeipigisha chapa kazi iliyoandikwa. Fasihi andishi imegawanyika katika kumbo mbili ambazo ni Nadhumu na Nathari. Nudhumu ni tungo za kishairi wakati nathari ni maandiko ya kimjazo yasiyofuata kanuni za kishairi. UHUSIANO WA FASIHI ANDISHI NA SIMULIZI Fasihi simulizi na andishi kuna mambo zinafanana, baadhi ya mambo hayo ni haya yafuatayo a) Zote hutumia ufundi wa lugha il...